Mit. 17:22-27 Swahili Union Version (SUV)

22. Moyo uliochangamka ni dawa nzuri;Bali roho iliyopondeka huikausha mifupa.

23. Asiye haki hutoa rushwa kifuani,Ili kuzipotosha njia za hukumu.

24. Hekima huwa machoni pake mwenye ufahamu;Bali macho ya mpumbavu huwa katika ncha za dunia.

25. Mwana mpumbavu ni huzuni kwa babaye,Na uchungu kwa mamaye aliyemzaa.

26. Tena kumwadhibu mwenye haki si vizuri;Wala si kwema kuwapiga wakuu kwa unyofu wao.

27. Azuiaye maneno yake ni mwenye maarifa;Na mwenye roho ya utulivu ana busara.

Mit. 17