21. Azaaye mpumbavu ni kwa huzuni yake mwenyewe;Wala baba wa mpumbavu hana furaha.
22. Moyo uliochangamka ni dawa nzuri;Bali roho iliyopondeka huikausha mifupa.
23. Asiye haki hutoa rushwa kifuani,Ili kuzipotosha njia za hukumu.
24. Hekima huwa machoni pake mwenye ufahamu;Bali macho ya mpumbavu huwa katika ncha za dunia.