Mit. 17:21-24 Swahili Union Version (SUV)

21. Azaaye mpumbavu ni kwa huzuni yake mwenyewe;Wala baba wa mpumbavu hana furaha.

22. Moyo uliochangamka ni dawa nzuri;Bali roho iliyopondeka huikausha mifupa.

23. Asiye haki hutoa rushwa kifuani,Ili kuzipotosha njia za hukumu.

24. Hekima huwa machoni pake mwenye ufahamu;Bali macho ya mpumbavu huwa katika ncha za dunia.

Mit. 17