Mit. 17:17-22 Swahili Union Version (SUV)

17. Rafiki hupenda sikuzote;Na ndugu amezaliwa kwa siku ya taabu.

18. Aliyepungukiwa na akili hupana mkono na mtu;Na kuwa mdhamini mbele ya mwenzake.

19. Apendaye ugomvi hupenda dhambi;Auinuaye sana mlango wake hutafuta uharibifu.

20. Mtu mwenye moyo wa ukaidi hatapata mema;Na mwenye ulimi wa upotofu huanguka katika misiba.

21. Azaaye mpumbavu ni kwa huzuni yake mwenyewe;Wala baba wa mpumbavu hana furaha.

22. Moyo uliochangamka ni dawa nzuri;Bali roho iliyopondeka huikausha mifupa.

Mit. 17