13. Yeye arudishaye mabaya badala ya mema,Mabaya hayataondoka nyumbani mwake.
14. Mwanzo wa ugomvi ni kama kutoboa penye maji;Basi acheni ugomvi kabla haujafurika.
15. Yeye asemaye kwamba asiye haki ana haki;naye asemaye kwamba mwenye haki hana haki;Hao wote wawili ni chukizo kwa BWANA.
16. Nini maana yake, mpumbavu kuwa na fedha mkononi mwake ya kununulia hekima,Ikiwa hana moyo wa ufahamu?
17. Rafiki hupenda sikuzote;Na ndugu amezaliwa kwa siku ya taabu.
18. Aliyepungukiwa na akili hupana mkono na mtu;Na kuwa mdhamini mbele ya mwenzake.