Mit. 17:12-22 Swahili Union Version (SUV)

12. Afadhali mtu akutwe na dubu aliyenyang’anywa watoto wake,Kuliko na mpumbavu katika upumbavu wake.

13. Yeye arudishaye mabaya badala ya mema,Mabaya hayataondoka nyumbani mwake.

14. Mwanzo wa ugomvi ni kama kutoboa penye maji;Basi acheni ugomvi kabla haujafurika.

15. Yeye asemaye kwamba asiye haki ana haki;naye asemaye kwamba mwenye haki hana haki;Hao wote wawili ni chukizo kwa BWANA.

16. Nini maana yake, mpumbavu kuwa na fedha mkononi mwake ya kununulia hekima,Ikiwa hana moyo wa ufahamu?

17. Rafiki hupenda sikuzote;Na ndugu amezaliwa kwa siku ya taabu.

18. Aliyepungukiwa na akili hupana mkono na mtu;Na kuwa mdhamini mbele ya mwenzake.

19. Apendaye ugomvi hupenda dhambi;Auinuaye sana mlango wake hutafuta uharibifu.

20. Mtu mwenye moyo wa ukaidi hatapata mema;Na mwenye ulimi wa upotofu huanguka katika misiba.

21. Azaaye mpumbavu ni kwa huzuni yake mwenyewe;Wala baba wa mpumbavu hana furaha.

22. Moyo uliochangamka ni dawa nzuri;Bali roho iliyopondeka huikausha mifupa.

Mit. 17