1. Afadhali mego kavu pamoja na utulivu,Kuliko nyumba yenye karamu nyingi pamoja na magomvi.
2. Mtumwa atendaye kwa busara atamtawala mwana atendaye mambo ya aibu;Tena atapata sehemu ya urithi kati ya ndugu.
3. Kalibuni kwa fedha, na tanuru kwa dhahabu;Bali BWANA huijaribu mioyo.
4. Mtenda mabaya husikiliza midomo ya uovu;Na mwongo hutega sikio lake kusikiliza ulimi wa madhara.
5. Amdhihakiye maskini humsuta Muumba wake;Naye aufurahiaye msiba hatakosa adhabu.
6. Wana wa wana ndio taji ya wazee,Na utukufu wa watoto ni baba zao.
7. Maneno mazuri hayapendezi kinywani mwa mpumbavu;Siuze midomo ya uongo kinywani mwa mkuu.