Mit. 17:1-10 Swahili Union Version (SUV)

1. Afadhali mego kavu pamoja na utulivu,Kuliko nyumba yenye karamu nyingi pamoja na magomvi.

2. Mtumwa atendaye kwa busara atamtawala mwana atendaye mambo ya aibu;Tena atapata sehemu ya urithi kati ya ndugu.

3. Kalibuni kwa fedha, na tanuru kwa dhahabu;Bali BWANA huijaribu mioyo.

4. Mtenda mabaya husikiliza midomo ya uovu;Na mwongo hutega sikio lake kusikiliza ulimi wa madhara.

5. Amdhihakiye maskini humsuta Muumba wake;Naye aufurahiaye msiba hatakosa adhabu.

6. Wana wa wana ndio taji ya wazee,Na utukufu wa watoto ni baba zao.

7. Maneno mazuri hayapendezi kinywani mwa mpumbavu;Siuze midomo ya uongo kinywani mwa mkuu.

8. Kipawa ni kama kito cha thamani machoni pake yeye aliye nacho;Kila kigeukapo hufanikiwa.

9. Afunikaye kosa hutafuta kupendwa;Bali yeye akashifuye neno hutenga rafiki.

10. Lawama hupenya moyoni mwa mwenye ufahamu,Kuliko mapigo mia moyoni mwa mpumbavu.

Mit. 17