4. BWANA amefanya kila kitu kwa kusudi lake;Naam, hata wabaya kwa siku ya ubaya.
5. Kila mwenye moyo wa kiburi ni chukizo kwa BWANA;Hakika, hatakosa adhabu.
6. Kwa rehema na kweli uovu husafishwa;Kwa kumcha BWANA watu hujiepusha na maovu.
7. Njia za mtu zikimpendeza BWANA,Hata adui zake huwapatanisha naye.
8. Afadhali mali kidogo pamoja na haki,Kuliko mapato mengi pamoja na udhalimu.
9. Moyo wa mtu huifikiri njia yake;Bali BWANA huziongoza hatua zake.
10. Kukata maneno huwa katika midomo ya mfalme;Kinywa chake hakitakosa katika hukumu.
11. Mizani ya haki na vitanga vyake ni vya BWANA;Mawe yote ya mfukoni ni kazi yake.
12. Wafalme wakitenda yasiyo haki ni chukizo;Maana kiti cha enzi huthibitika kwa haki.
13. Midomo ya haki ni furaha ya wafalme;Nao humpenda yeye asemaye yaliyo sawa.
14. Hasira ya mfalme ni kama wajumbe wa mauti;Lakini mtu mwenye hekima ataituliza.
15. Kuna uhai katika nuru ya uso wa mfalme,Na fadhili zake ni kama wingu la masika.
16. Si afadhali kupata hekima kuliko dhahabu?Naam, yafaa kuchagua ufahamu kuliko fedha.