Mit. 16:3-6 Swahili Union Version (SUV)

3. Mkabidhi BWANA kazi zako,Na mawazo yako yatathibitika.

4. BWANA amefanya kila kitu kwa kusudi lake;Naam, hata wabaya kwa siku ya ubaya.

5. Kila mwenye moyo wa kiburi ni chukizo kwa BWANA;Hakika, hatakosa adhabu.

6. Kwa rehema na kweli uovu husafishwa;Kwa kumcha BWANA watu hujiepusha na maovu.

Mit. 16