3. Mkabidhi BWANA kazi zako,Na mawazo yako yatathibitika.
4. BWANA amefanya kila kitu kwa kusudi lake;Naam, hata wabaya kwa siku ya ubaya.
5. Kila mwenye moyo wa kiburi ni chukizo kwa BWANA;Hakika, hatakosa adhabu.
6. Kwa rehema na kweli uovu husafishwa;Kwa kumcha BWANA watu hujiepusha na maovu.