Mit. 16:21-27 Swahili Union Version (SUV)

21. Aliye na hekima moyoni ataitwa mwenye busara;Utamu wa maneno huongeza elimu.

22. Ufahamu ni chemchemi ya uzima kwake aliye nao;Bali kufundishwa kwa wapumbavu ni upuzi wao.

23. Moyo wake mwenye hekima hufundisha kinywa chake;Huzidisha elimu ya midomo yake.

24. Maneno yapendezayo ni kama sega la asali;Ni tamu nafsini, na afya mifupani.

25. Iko njia ionekanayo kuwa sawa machoni pa mtu;Lakini mwisho wake ni njia za mauti.

26. Nafsi yake mfanya kazi hujifanyia kazi;Maana kinywa chake humtia bidii.

27. Mtu asiyefaa kitu huchimba shimo la madhara;Katika midomo yake mna moto uteketezao.

Mit. 16