21. Aliye na hekima moyoni ataitwa mwenye busara;Utamu wa maneno huongeza elimu.
22. Ufahamu ni chemchemi ya uzima kwake aliye nao;Bali kufundishwa kwa wapumbavu ni upuzi wao.
23. Moyo wake mwenye hekima hufundisha kinywa chake;Huzidisha elimu ya midomo yake.
24. Maneno yapendezayo ni kama sega la asali;Ni tamu nafsini, na afya mifupani.
25. Iko njia ionekanayo kuwa sawa machoni pa mtu;Lakini mwisho wake ni njia za mauti.