Mit. 16:17-32 Swahili Union Version (SUV)

17. Njia kuu ya mwenye haki ni kujitenga na uovu;Yeye ashikaye njia yake huihifadhi nafsi yake.

18. Kiburi hutangulia uangamivu;Na roho yenye kutakabari hutangulia maanguko.

19. Afadhali kuwa na roho ya unyenyekevu pamoja na maskini,Kuliko kugawanya nyara pamoja na wenye kiburi.

20. Atakayelitafakari neno atapata mema;Na kila amwaminiye BWANA ana heri.

21. Aliye na hekima moyoni ataitwa mwenye busara;Utamu wa maneno huongeza elimu.

22. Ufahamu ni chemchemi ya uzima kwake aliye nao;Bali kufundishwa kwa wapumbavu ni upuzi wao.

23. Moyo wake mwenye hekima hufundisha kinywa chake;Huzidisha elimu ya midomo yake.

24. Maneno yapendezayo ni kama sega la asali;Ni tamu nafsini, na afya mifupani.

25. Iko njia ionekanayo kuwa sawa machoni pa mtu;Lakini mwisho wake ni njia za mauti.

26. Nafsi yake mfanya kazi hujifanyia kazi;Maana kinywa chake humtia bidii.

27. Mtu asiyefaa kitu huchimba shimo la madhara;Katika midomo yake mna moto uteketezao.

28. Mtu mshupavu huondokesha fitina;Na mchongezi huwafarakanisha rafiki.

29. Mtu mkali humshawishi mwenzake;Humwongoza katika njia isiyo njema.

30. Afumbaye macho, kusudi lake ni kuwaza yaliyopotoka;Aikazaye midomo yake hutokeza mabaya.

31. Kichwa chenye mvi ni taji ya utukufu,Kama kikionekana katika njia ya haki.

32. Asiye mwepesi wa hasira ni mwema kuliko shujaa;Na mtu aitawalaye roho yake kuliko mtu atekaye mji.

Mit. 16