13. Midomo ya haki ni furaha ya wafalme;Nao humpenda yeye asemaye yaliyo sawa.
14. Hasira ya mfalme ni kama wajumbe wa mauti;Lakini mtu mwenye hekima ataituliza.
15. Kuna uhai katika nuru ya uso wa mfalme,Na fadhili zake ni kama wingu la masika.
16. Si afadhali kupata hekima kuliko dhahabu?Naam, yafaa kuchagua ufahamu kuliko fedha.
17. Njia kuu ya mwenye haki ni kujitenga na uovu;Yeye ashikaye njia yake huihifadhi nafsi yake.
18. Kiburi hutangulia uangamivu;Na roho yenye kutakabari hutangulia maanguko.
19. Afadhali kuwa na roho ya unyenyekevu pamoja na maskini,Kuliko kugawanya nyara pamoja na wenye kiburi.
20. Atakayelitafakari neno atapata mema;Na kila amwaminiye BWANA ana heri.
21. Aliye na hekima moyoni ataitwa mwenye busara;Utamu wa maneno huongeza elimu.
22. Ufahamu ni chemchemi ya uzima kwake aliye nao;Bali kufundishwa kwa wapumbavu ni upuzi wao.
23. Moyo wake mwenye hekima hufundisha kinywa chake;Huzidisha elimu ya midomo yake.
24. Maneno yapendezayo ni kama sega la asali;Ni tamu nafsini, na afya mifupani.
25. Iko njia ionekanayo kuwa sawa machoni pa mtu;Lakini mwisho wake ni njia za mauti.
26. Nafsi yake mfanya kazi hujifanyia kazi;Maana kinywa chake humtia bidii.
27. Mtu asiyefaa kitu huchimba shimo la madhara;Katika midomo yake mna moto uteketezao.
28. Mtu mshupavu huondokesha fitina;Na mchongezi huwafarakanisha rafiki.