1. Maandalio ya moyo ni ya mwanadamu;Bali jawabu la ulimi hutoka kwa BWANA.
2. Njia zote za mtu ni safi machoni pake mwenyewe;Bali BWANA huzipima roho za watu.
3. Mkabidhi BWANA kazi zako,Na mawazo yako yatathibitika.
4. BWANA amefanya kila kitu kwa kusudi lake;Naam, hata wabaya kwa siku ya ubaya.
5. Kila mwenye moyo wa kiburi ni chukizo kwa BWANA;Hakika, hatakosa adhabu.
6. Kwa rehema na kweli uovu husafishwa;Kwa kumcha BWANA watu hujiepusha na maovu.
7. Njia za mtu zikimpendeza BWANA,Hata adui zake huwapatanisha naye.
8. Afadhali mali kidogo pamoja na haki,Kuliko mapato mengi pamoja na udhalimu.