Mit. 16:1-4 Swahili Union Version (SUV)

1. Maandalio ya moyo ni ya mwanadamu;Bali jawabu la ulimi hutoka kwa BWANA.

2. Njia zote za mtu ni safi machoni pake mwenyewe;Bali BWANA huzipima roho za watu.

3. Mkabidhi BWANA kazi zako,Na mawazo yako yatathibitika.

4. BWANA amefanya kila kitu kwa kusudi lake;Naam, hata wabaya kwa siku ya ubaya.

Mit. 16