1. Maandalio ya moyo ni ya mwanadamu;Bali jawabu la ulimi hutoka kwa BWANA.
2. Njia zote za mtu ni safi machoni pake mwenyewe;Bali BWANA huzipima roho za watu.
3. Mkabidhi BWANA kazi zako,Na mawazo yako yatathibitika.
4. BWANA amefanya kila kitu kwa kusudi lake;Naam, hata wabaya kwa siku ya ubaya.