Mit. 15:5-12 Swahili Union Version (SUV)

5. Mpumbavu hudharau kurudiwa na babaye;Bali yeye aangaliaye maonyo hupata busara.

6. Katika nyumba ya mwenye haki mna akiba nyingi;Bali mapato ya mtu mbaya huwa taabu tu.

7. Midomo ya mwenye haki hueneza maarifa;Bali moyo wa mpumbavu haufanyi hivyo.

8. Sadaka ya mtu mbaya ni chukizo kwa BWANA;Bali maombi ya mtu mnyofu ni furaha yake.

9. Njia ya mtu mbaya ni chukizo kwa BWANA;Bali humpenda mtu afuatiaye wema.

10. Adhabu kali ina yeye aiachaye njia;Naye achukiaye kukemewa atakufa.

11. Kuzimu na Uharibifu vi wazi mbele za BWANA;Si zaidi basi, mioyo ya wanadamu?

12. Mwenye mzaha hapendi kukaripiwa;Wala yeye hawaendei wenye hekima.

Mit. 15