3. Macho ya BWANA yako kila mahali;Yakimchunguza mbaya na mwema.
4. Ulimi safi ni mti wa uzima;Bali ukorofi wa ulimi huvunja moyo.
5. Mpumbavu hudharau kurudiwa na babaye;Bali yeye aangaliaye maonyo hupata busara.
6. Katika nyumba ya mwenye haki mna akiba nyingi;Bali mapato ya mtu mbaya huwa taabu tu.
7. Midomo ya mwenye haki hueneza maarifa;Bali moyo wa mpumbavu haufanyi hivyo.
8. Sadaka ya mtu mbaya ni chukizo kwa BWANA;Bali maombi ya mtu mnyofu ni furaha yake.
9. Njia ya mtu mbaya ni chukizo kwa BWANA;Bali humpenda mtu afuatiaye wema.
10. Adhabu kali ina yeye aiachaye njia;Naye achukiaye kukemewa atakufa.
11. Kuzimu na Uharibifu vi wazi mbele za BWANA;Si zaidi basi, mioyo ya wanadamu?
12. Mwenye mzaha hapendi kukaripiwa;Wala yeye hawaendei wenye hekima.
13. Moyo wa furaha huchangamsha uso;Bali kwa huzuni ya moyo roho hupondeka.
14. Moyo wa mwenye ufahamu hutafuta maarifa;Bali kinywa cha wapumbavu hula upumbavu.