Mit. 15:3-14 Swahili Union Version (SUV)

3. Macho ya BWANA yako kila mahali;Yakimchunguza mbaya na mwema.

4. Ulimi safi ni mti wa uzima;Bali ukorofi wa ulimi huvunja moyo.

5. Mpumbavu hudharau kurudiwa na babaye;Bali yeye aangaliaye maonyo hupata busara.

6. Katika nyumba ya mwenye haki mna akiba nyingi;Bali mapato ya mtu mbaya huwa taabu tu.

7. Midomo ya mwenye haki hueneza maarifa;Bali moyo wa mpumbavu haufanyi hivyo.

8. Sadaka ya mtu mbaya ni chukizo kwa BWANA;Bali maombi ya mtu mnyofu ni furaha yake.

9. Njia ya mtu mbaya ni chukizo kwa BWANA;Bali humpenda mtu afuatiaye wema.

10. Adhabu kali ina yeye aiachaye njia;Naye achukiaye kukemewa atakufa.

11. Kuzimu na Uharibifu vi wazi mbele za BWANA;Si zaidi basi, mioyo ya wanadamu?

12. Mwenye mzaha hapendi kukaripiwa;Wala yeye hawaendei wenye hekima.

13. Moyo wa furaha huchangamsha uso;Bali kwa huzuni ya moyo roho hupondeka.

14. Moyo wa mwenye ufahamu hutafuta maarifa;Bali kinywa cha wapumbavu hula upumbavu.

Mit. 15