Mit. 15:26-30 Swahili Union Version (SUV)

26. Mashauri mabaya ni chukizo kwa BWANA;Bali maneno yapendezayo ni safi.

27. Atamaniye faida huifadhaisha nyumba yake mwenyewe;Bali achukiaye zawadi ataishi.

28. Moyo wa mwenye haki hufikiri jinsi atakavyojibu;Bali kinywa cha wasio haki humwaga mabaya.

29. BWANA yu mbali na wasio haki;Bali huisikia sala ya mwenye haki.

30. Mng’ao wa macho huufurahisha moyo;Habari njema huinenepesha mifupa.

Mit. 15