24. Kwa mtu mwenye akili njia ya uhai huenda juu;Ili atoke katika kuzimu chini.
25. BWANA ataing’oa nyumba ya mwenye kiburi;Bali atauthibitisha mpaka wa mjane.
26. Mashauri mabaya ni chukizo kwa BWANA;Bali maneno yapendezayo ni safi.
27. Atamaniye faida huifadhaisha nyumba yake mwenyewe;Bali achukiaye zawadi ataishi.
28. Moyo wa mwenye haki hufikiri jinsi atakavyojibu;Bali kinywa cha wasio haki humwaga mabaya.
29. BWANA yu mbali na wasio haki;Bali huisikia sala ya mwenye haki.
30. Mng’ao wa macho huufurahisha moyo;Habari njema huinenepesha mifupa.
31. Sikio lisikilizalo lawama yenye uhaiLitakaa kati yao wenye hekima.
32. Akataaye maonyo huidharau nafsi yake mwenyewe;Bali yeye asikilizaye lawama hujipatia ufahamu.