Mit. 15:23-32 Swahili Union Version (SUV)

23. Mtu hulifurahia jibu la kinywa chake;Na neno linenwalo wakati wa kufaa ni jema kama nini!

24. Kwa mtu mwenye akili njia ya uhai huenda juu;Ili atoke katika kuzimu chini.

25. BWANA ataing’oa nyumba ya mwenye kiburi;Bali atauthibitisha mpaka wa mjane.

26. Mashauri mabaya ni chukizo kwa BWANA;Bali maneno yapendezayo ni safi.

27. Atamaniye faida huifadhaisha nyumba yake mwenyewe;Bali achukiaye zawadi ataishi.

28. Moyo wa mwenye haki hufikiri jinsi atakavyojibu;Bali kinywa cha wasio haki humwaga mabaya.

29. BWANA yu mbali na wasio haki;Bali huisikia sala ya mwenye haki.

30. Mng’ao wa macho huufurahisha moyo;Habari njema huinenepesha mifupa.

31. Sikio lisikilizalo lawama yenye uhaiLitakaa kati yao wenye hekima.

32. Akataaye maonyo huidharau nafsi yake mwenyewe;Bali yeye asikilizaye lawama hujipatia ufahamu.

Mit. 15