Mit. 15:16-20 Swahili Union Version (SUV)

16. Kuwa na mali chache pamoja na kumcha BWANA;Ni bora kuliko mali nyingi pamoja na taabu.

17. Chakula cha mboga penye mapendano;Ni bora kuliko ng’ombe aliyenona pamoja na kuchukiana.

18. Mtu wa hasira huchochea ugomvi;Bali asiye mwepesi wa hasira hutuliza mashindano.

19. Njia ya mtu mvivu ni kama boma la miiba;Bali mapito yao wenye unyofu hufanyika njia kuu.

20. Mwana mwenye hekima humfurahisha babaye;Bali mpumbavu humdharau mamaye.

Mit. 15