15. Siku zote za mtu ateswaye ni mbaya;Bali ukunjufu wa moyo ni karamu ya daima.
16. Kuwa na mali chache pamoja na kumcha BWANA;Ni bora kuliko mali nyingi pamoja na taabu.
17. Chakula cha mboga penye mapendano;Ni bora kuliko ng’ombe aliyenona pamoja na kuchukiana.
18. Mtu wa hasira huchochea ugomvi;Bali asiye mwepesi wa hasira hutuliza mashindano.
19. Njia ya mtu mvivu ni kama boma la miiba;Bali mapito yao wenye unyofu hufanyika njia kuu.
20. Mwana mwenye hekima humfurahisha babaye;Bali mpumbavu humdharau mamaye.
21. Upumbavu ni furaha kwake aliyepungukiwa na akili;Bali mwenye ufahamu huunyosha mwenendo wake.
22. Pasipo mashauri makusudi hubatilika;Bali kwa wingi wa washauri huthibithika.
23. Mtu hulifurahia jibu la kinywa chake;Na neno linenwalo wakati wa kufaa ni jema kama nini!
24. Kwa mtu mwenye akili njia ya uhai huenda juu;Ili atoke katika kuzimu chini.
25. BWANA ataing’oa nyumba ya mwenye kiburi;Bali atauthibitisha mpaka wa mjane.
26. Mashauri mabaya ni chukizo kwa BWANA;Bali maneno yapendezayo ni safi.
27. Atamaniye faida huifadhaisha nyumba yake mwenyewe;Bali achukiaye zawadi ataishi.