10. Adhabu kali ina yeye aiachaye njia;Naye achukiaye kukemewa atakufa.
11. Kuzimu na Uharibifu vi wazi mbele za BWANA;Si zaidi basi, mioyo ya wanadamu?
12. Mwenye mzaha hapendi kukaripiwa;Wala yeye hawaendei wenye hekima.
13. Moyo wa furaha huchangamsha uso;Bali kwa huzuni ya moyo roho hupondeka.
14. Moyo wa mwenye ufahamu hutafuta maarifa;Bali kinywa cha wapumbavu hula upumbavu.
15. Siku zote za mtu ateswaye ni mbaya;Bali ukunjufu wa moyo ni karamu ya daima.
16. Kuwa na mali chache pamoja na kumcha BWANA;Ni bora kuliko mali nyingi pamoja na taabu.
17. Chakula cha mboga penye mapendano;Ni bora kuliko ng’ombe aliyenona pamoja na kuchukiana.
18. Mtu wa hasira huchochea ugomvi;Bali asiye mwepesi wa hasira hutuliza mashindano.
19. Njia ya mtu mvivu ni kama boma la miiba;Bali mapito yao wenye unyofu hufanyika njia kuu.
20. Mwana mwenye hekima humfurahisha babaye;Bali mpumbavu humdharau mamaye.
21. Upumbavu ni furaha kwake aliyepungukiwa na akili;Bali mwenye ufahamu huunyosha mwenendo wake.
22. Pasipo mashauri makusudi hubatilika;Bali kwa wingi wa washauri huthibithika.