Mit. 15:1-3 Swahili Union Version (SUV)

1. Jawabu la upole hugeuza hasira;Bali neno liumizalo huchochea ghadhabu.

2. Ulimi wa mwenye hekima hutamka maarifa vizuri;Bali vinywa vya wapumbavu humwaga upumbavu.

3. Macho ya BWANA yako kila mahali;Yakimchunguza mbaya na mwema.

Mit. 15