9. Nuru ya mwenye haki yang’aa sana;Bali taa ya mtu mbaya itazimika.
10. Kiburi huleta mashindano tu;Bali hekima hukaa nao wanaoshauriana.
11. Mali iliyopatikana kwa haraka itapunguka;Bali yeye achumaye kidogo kidogo atazidishiwa.
12. Kilichotarajiwa kikikawia kuja, moyo huugua.Bali haja ya mtu ikipatikana, ni mti wa uzima.
13. Kila alidharauye neno hujiletea uharibifu;Bali yeye aiogopaye amri atapewa thawabu.
14. Sheria ya mwenye akili ni chemchemi ya uzima,Ili kuepukana na tanzi za mauti.