13. Kila alidharauye neno hujiletea uharibifu;Bali yeye aiogopaye amri atapewa thawabu.
14. Sheria ya mwenye akili ni chemchemi ya uzima,Ili kuepukana na tanzi za mauti.
15. Ufahamu mwema huleta upendeleo;Bali njia ya haini huparuza.
16. Kila aliye na busara hutenda kazi kwa maarifa;Bali mpumbavu hueneza upumbavu.
17. Mjumbe mbaya huanguka maovuni;Bali mjumbe mwaminifu ni afya.
18. Umaskini na fedheha zitampata yeye akataaye kurudiwa;Bali yeye aangaliaye maonyo ataheshimiwa.
19. Haja iliyopatikana ni tamu nafsini mwa mtu;Bali kujitenga na maovu ni chukizo kwa wapumbavu.