Mit. 12:8-14 Swahili Union Version (SUV)

8. Mtu atasifiwa kwa kadiri ya akili zake;Bali mwenye moyo wa ukaidi atadharauliwa.

9. Afadhali mtu anayedharauliwa, ikiwa ana mtumwa,Kuliko ajisifuye, ikiwa anahitaji chakula.

10. Mwenye haki huufikiri uhai wa mnyama wake;Bali huruma za mtu mwovu ni ukatili.

11. Alimaye shamba lake atakuwa na chakula tele;Bali afuataye mambo ya upuzi hana ufahamu.

12. Asiye haki hutamani nyavu za wabaya;Bali shina lao wenye haki huleta matunda.

13. Katika kosa la midomo kuna mtego kwa mbaya;Bali mwenye haki atatoka katika taabu.

14. Mtu atashiba mema kwa matunda ya kinywa chake;Na atarudishiwa matendo ya mikono yake.

Mit. 12