Mit. 1:1-6 Swahili Union Version (SUV)

1. Mithali za Sulemani, mwana wa Daudi, mfalme wa Israeli.

2. Kujua hekima na adabu; kutambua maneno ya ufahamu;

3. kufundishwa matendo ya busara, katika haki na hukumu na adili.

4. Kuwapa wajinga werevu, na kijana maarifa na hadhari;

5. mwenye hekima asikie na kuongezewa elimu, na mwenye ufahamu ayafikie mashauri yenye njia.

6. Kufahamu mithali na kitendawili, na maneno ya wenye hekima na mafumbo yao.

Mit. 1