Mik. 5:12-15 Swahili Union Version (SUV)

12. nami nitakatilia mbali uchawi, usiwe mkononi mwako; wala hutakuwa tena na watu wenye kutabana;

13. nami nitakatilia mbali sanamu zako na nguzo zako, zitoke kati yako; wala hutaiabudu tena kazi ya mikono yako.

14. Nami nitayang’oa maashera yenu, yasiwe kati yako; nami nitaiangamiza miji yako.

15. Nami nitajilipiza kisasi katika hasira na ghadhabu juu ya mataifa wasiosikiliza.

Mik. 5