Mik. 2:11-13 Swahili Union Version (SUV)

11. Mtu akienda kwa roho ya uongo, akinena maneno ya uongo, akisema, Nitakutabiria habari ya mvinyo na kileo; mtu huyu atakuwa nabii wao watu hawa.

12. Hakika nitakukusanya, Ee Yakobo, nyote pia;Bila shaka nitawakusanya waliobaki wa Israeli;Nitawaweka pamoja kama kondoo wa Bozra;Kama kundi la kondoo kati ya malisho yao;Watafanya mvumo kwa wingi wa watu;

13. Avunjaye amekwea juu mbele yao;Wamebomoa mahali, wakapita mpaka langoni,Wakatoka nje huko;Mfalme wao naye amepita akiwatangulia,Naye BWANA ametangulia mbele yao.

Mik. 2