Mhu. 3:3-9 Swahili Union Version (SUV)

3. Wakati wa kuua, na wakati wa kupoza;Wakati wa kubomoa, na wakati wa kujenga;

4. Wakati wa kulia, na wakati wa kucheka;Wakati wa kuomboleza, na wakati wa kucheza;

5. Wakati wa kutupa mawe, na wakati wa kukusanya mawe;Wakati wa kukumbatia, na wakati wa kutokumbatia;

6. Wakati wa kutafuta, na wakati wa kupoteza;Wakati wa kuweka, na wakati wa kutupa;

7. Wakati wa kurarua, na wakati wa kushona;Wakati wa kunyamaza, na wakati wa kunena;

8. Wakati wa kupenda, na wakati wa kuchukia;Wakati wa vita, na wakati wa amani.

9. Je! Mtendaji anayo faida gani katika yale anayojishughulisha nayo?

Mhu. 3