1. Kwa kila jambo kuna majira yake,Na wakati kwa kila kusudi chini ya mbingu.
2. Wakati wa kuzaliwa, na wakati wa kufa;Wakati wa kupanda, na wakati wa kung’oa yaliyopandwa;
3. Wakati wa kuua, na wakati wa kupoza;Wakati wa kubomoa, na wakati wa kujenga;
4. Wakati wa kulia, na wakati wa kucheka;Wakati wa kuomboleza, na wakati wa kucheza;
5. Wakati wa kutupa mawe, na wakati wa kukusanya mawe;Wakati wa kukumbatia, na wakati wa kutokumbatia;
6. Wakati wa kutafuta, na wakati wa kupoteza;Wakati wa kuweka, na wakati wa kutupa;
7. Wakati wa kurarua, na wakati wa kushona;Wakati wa kunyamaza, na wakati wa kunena;
8. Wakati wa kupenda, na wakati wa kuchukia;Wakati wa vita, na wakati wa amani.
9. Je! Mtendaji anayo faida gani katika yale anayojishughulisha nayo?