Mhu. 3:1-9 Swahili Union Version (SUV)

1. Kwa kila jambo kuna majira yake,Na wakati kwa kila kusudi chini ya mbingu.

2. Wakati wa kuzaliwa, na wakati wa kufa;Wakati wa kupanda, na wakati wa kung’oa yaliyopandwa;

3. Wakati wa kuua, na wakati wa kupoza;Wakati wa kubomoa, na wakati wa kujenga;

4. Wakati wa kulia, na wakati wa kucheka;Wakati wa kuomboleza, na wakati wa kucheza;

5. Wakati wa kutupa mawe, na wakati wa kukusanya mawe;Wakati wa kukumbatia, na wakati wa kutokumbatia;

6. Wakati wa kutafuta, na wakati wa kupoteza;Wakati wa kuweka, na wakati wa kutupa;

7. Wakati wa kurarua, na wakati wa kushona;Wakati wa kunyamaza, na wakati wa kunena;

8. Wakati wa kupenda, na wakati wa kuchukia;Wakati wa vita, na wakati wa amani.

9. Je! Mtendaji anayo faida gani katika yale anayojishughulisha nayo?

Mhu. 3