Mhu. 3:1-12 Swahili Union Version (SUV)

1. Kwa kila jambo kuna majira yake,Na wakati kwa kila kusudi chini ya mbingu.

2. Wakati wa kuzaliwa, na wakati wa kufa;Wakati wa kupanda, na wakati wa kung’oa yaliyopandwa;

3. Wakati wa kuua, na wakati wa kupoza;Wakati wa kubomoa, na wakati wa kujenga;

4. Wakati wa kulia, na wakati wa kucheka;Wakati wa kuomboleza, na wakati wa kucheza;

5. Wakati wa kutupa mawe, na wakati wa kukusanya mawe;Wakati wa kukumbatia, na wakati wa kutokumbatia;

6. Wakati wa kutafuta, na wakati wa kupoteza;Wakati wa kuweka, na wakati wa kutupa;

7. Wakati wa kurarua, na wakati wa kushona;Wakati wa kunyamaza, na wakati wa kunena;

8. Wakati wa kupenda, na wakati wa kuchukia;Wakati wa vita, na wakati wa amani.

9. Je! Mtendaji anayo faida gani katika yale anayojishughulisha nayo?

10. Nimeiona taabu ambayo Mungu amewapa wanadamu, ili kutaabika ndani yake.

11. Kila kitu amekifanya kizuri kwa wakati wake; tena ameiweka hiyo milele ndani ya mioyo yao; ila kwa jinsi mwanadamu asivyoweza kuivumbua kazi ya Mungu anayoifanya, tangu mwanzo hata mwisho.

12. Mimi najua ya kwamba hakuna jema kwao kupita kufurahi, na kufanya mema maadamu wanaishi.

Mhu. 3