Mhu. 2:4-8 Swahili Union Version (SUV)

4. Nikajifanyizia kazi zilizo kubwa; nikajijengea nyumba; nikajipandia mashamba ya mizabibu;

5. nikajifanyizia bustani na viunga, na kuipanda humo miti yenye matunda ya kila namna;

6. nikajifanyizia birika za maji, ya kuunyweshea mwitu mlimopandwa miti michanga.

7. Nami nikanunua watumwa na wajakazi, nikawa na wazalia nyumbani mwangu; tena nikawa na mali nyingi za ng’ombe na kondoo, kupita wote walionitangulia katika Yerusalemu;

8. tena nikajikusanyia fedha na dhahabu, na tunu za kifalme na za kutoka katika majimbo. Nikajipatia waimbaji, waume kwa wake, nao wale ambao wanadamu wanawatunuka, masuria wengi sana.

Mhu. 2