Mhu. 12:5-14 Swahili Union Version (SUV)

5. Naam, wataogopa kilichoinukaNa vitisho vitakuwapo njiani;Na mlozi utachanua maua;Na panzi atakuwa ni mzigo mzito;Na pilipili hoho itapasuka;Maana mtu aiendea nyumba yake ya milele,Nao waombolezao wazunguka njiani.

6. Kabla haijakatika kamba ya fedha;Au kuvunjwa bakuli la dhahabu;Au mtungi kuvunjika kisimani;Au gurudumu kuvunjika birikani;

7. Nayo mavumbi kuirudia nchi kama yalivyokuwa,Nayo roho kumrudia Mungu aliyeitoa.

8. Mhubiri asema, Ubatili mtupu; mambo yote ni ubatili!

9. Walakini, kwa sababu huyo Mhubiri alikuwa na hekima, aliendelea kuwafundisha watu maarifa, naam, akatafakari, akatafuta-tafuta, akatunga mithali nyingi.

10. Huyo Mhubiri akatafuta-tafuta ili apate kuona maneno yapendezayo, na yale yaliyoandikwa kwa unyofu, yaani, maneno ya kweli.

11. Maneno yao wenye hekima huwa mfano wa michokoo; na kama misumari iliyogongomewa sana; ndivyo yalivyo maneno yao walio wakuu wa makusanyiko, ambayo yatoka kwa mchungaji mmoja.

12. Tena, zaidi ya hayo, mwanangu, kubali maonyo; hakuna mwisho wo wote wa kutunga vitabu vingi; na kusoma sana huuchosha mwili.

13. Hii ndiyo jumla ya maneno; yote yamekwisha sikiwa;Mche Mungu, nawe uzishike amri zake,Maana kwa jumla ndiyo impasayo mtu.

14. Kwa maana Mungu ataleta hukumuni kila kazi, pamoja na kila neno la siri, likiwa jema au likiwa baya.

Mhu. 12