9. Mwenye kuchonga mawe ataumizwa kwayo;Naye apasuaye miti huona hatari katika hiyo.
10. Iwapo chuma hakipati, wala mtu hakinoi;Ndipo hana budi kutumia nguvu zaidi. Walakini yafaa kutumia hekima, na kufanikiwa.
11. Nyoka akiuma asijatumbuizwa,Basi hakuna faida ya mtumbuizi.
12. Maneno ya kinywa chake mwenye hekima yana neema;Bali midomo ya mpumbavu itammeza nafsi yake.
13. Mwanzo wa maneno ya kinywa chake ni upuuzi; na mwisho wa usemi wake ni wazimu wenye hatari.
14. Tena, upumbavu huongeza maneno; lakini mwanadamu hajui yatakayokuwako; nayo yatakayokuwa baada yake, ni nani awezaye kumweleza?
15. Kazi yao wapumbavu huwachosha kila mmoja,Maana hajui hata njia ya kuuendea mji.