Mhu. 10:9-15 Swahili Union Version (SUV)

9. Mwenye kuchonga mawe ataumizwa kwayo;Naye apasuaye miti huona hatari katika hiyo.

10. Iwapo chuma hakipati, wala mtu hakinoi;Ndipo hana budi kutumia nguvu zaidi. Walakini yafaa kutumia hekima, na kufanikiwa.

11. Nyoka akiuma asijatumbuizwa,Basi hakuna faida ya mtumbuizi.

12. Maneno ya kinywa chake mwenye hekima yana neema;Bali midomo ya mpumbavu itammeza nafsi yake.

13. Mwanzo wa maneno ya kinywa chake ni upuuzi; na mwisho wa usemi wake ni wazimu wenye hatari.

14. Tena, upumbavu huongeza maneno; lakini mwanadamu hajui yatakayokuwako; nayo yatakayokuwa baada yake, ni nani awezaye kumweleza?

15. Kazi yao wapumbavu huwachosha kila mmoja,Maana hajui hata njia ya kuuendea mji.

Mhu. 10