Mhu. 10:5-15 Swahili Union Version (SUV)

5. Liko baa nililoliona chini ya jua, nalo ni kama kosa litokalo kwake yeye atawalaye;

6. ya kuwa upumbavu huwekwa mahali pa juu sana, nao wakwasi hukaa mahali pa chini.

7. Mimi nimeona watumwa wamepanda farasi, na wakuu wakienda kwa miguu juu ya nchi kama watumwa.

8. Mwenye kuchimba shimo atatumbukia ndani yake;Na yeye abomoaye boma, nyoka atamwuma.

9. Mwenye kuchonga mawe ataumizwa kwayo;Naye apasuaye miti huona hatari katika hiyo.

10. Iwapo chuma hakipati, wala mtu hakinoi;Ndipo hana budi kutumia nguvu zaidi. Walakini yafaa kutumia hekima, na kufanikiwa.

11. Nyoka akiuma asijatumbuizwa,Basi hakuna faida ya mtumbuizi.

12. Maneno ya kinywa chake mwenye hekima yana neema;Bali midomo ya mpumbavu itammeza nafsi yake.

13. Mwanzo wa maneno ya kinywa chake ni upuuzi; na mwisho wa usemi wake ni wazimu wenye hatari.

14. Tena, upumbavu huongeza maneno; lakini mwanadamu hajui yatakayokuwako; nayo yatakayokuwa baada yake, ni nani awezaye kumweleza?

15. Kazi yao wapumbavu huwachosha kila mmoja,Maana hajui hata njia ya kuuendea mji.

Mhu. 10