Mhu. 1:6-9 Swahili Union Version (SUV)

6. Upepo huvuma kusi, hugeuka kuwa kaskazi; hugeuka daima katika mwendo wake, na upepo huyarudia mazunguko yake.

7. Mito yote huingia baharini, walakini bahari haijai; huko iendako mito, ndiko irudiko tena.

8. Mambo yote yamejaa uchovu usioneneka, jicho halishibi kuona, wala sikio halikinai kusikia.

9. Yaliyokuwako ndiyo yatakayokuwako; na yaliyotendeka ndiyo yatakayotendeka; wala jambo jipya hakuna chini ya jua.

Mhu. 1