Mhu. 1:14-18 Swahili Union Version (SUV)

14. Nimeziona kazi zote zifanywazo chini ya jua; na, tazama, mambo yote ni ubatili na kujilisha upepo.

15. Yaliyopotoka hayawezi kunyoshwa,Wala yasiyokuwapo hayahesabiki.

16. Nikatafakari nikisema, Nimejipatia hekima nyingi kupita wote walionitangulia katika Yerusalemu; naam, moyo wangu umeona kwa wingi hekima na maarifa.

17. Nikatia moyo wangu ili kuijua hekima, na kujua wazimu na upumbavu; nikatambua ya kwamba hayo yote nayo ni kujilisha upepo.

18. Yaani,Katika wingi wa hekima mna wingi wa huzuni;Naye aongezaye maarifa huongeza masikitiko.

Mhu. 1