48. Ila Yeye aliye juu hakai katika nyumba zilizofanywa kwa mikono, kama vile asemavyo nabii,
49. Mbingu ni kiti changu cha enzi,Na nchi ni pa kuwekea miguu yangu;Ni nyumba gani mtakayonijengea? Asema Bwana,
50. Au ni mahali gani nitakapostarehe?Si mkono wangu uliofanya haya yote?
51. Enyi wenye shingo gumu, msiotahiriwa mioyo wala masikio, siku zote mnampinga Roho Mtakatifu; kama baba zenu walivyofanya, na ninyi ni vivyo hivyo.
52. Ni yupi katika manabii ambaye baba zenu hawakumwudhi? Nao waliwaua wale waliotabiri habari za kuja kwake yule Mwenye Haki; ambaye ninyi sasa mmekuwa wasaliti wake, mkamwua;
53. ninyi mlioipokea torati kwa agizo la malaika msiishike.
54. Basi waliposikia maneno haya, wakachomwa mioyo, wakamsagia meno.