Mdo 7:11-22 Swahili Union Version (SUV)

11. Basi kukawa njaa katika nchi yote ya Misri na Kanaani, na dhiki nyingi, wala baba zetu hawakupata chakula cha kuwatosha.

12. Hata Yakobo aliposikia ya kwamba huko Misri kuna nafaka, akawatuma baba zetu mara ya kwanza.

13. Hata safari ya pili Yusufu akajitambulisha kwa ndugu zake, jamaa ya Yusufu ikawa dhahiri kwa Farao.

14. Yusufu akatuma watu akamwita Yakobo babaye na jamaa zake wote pia, watu sabini na watano.

15. Basi Yakobo akashuka mpaka Misri; akafa yeye na baba zetu;

16. wakachukuliwa mpaka Shekemu wakazikwa katika kaburi lile, ambalo Ibrahimu alilinunua kwa kima cha fedha kwa wana wa Hamori, huko Shekemu.

17. Basi wakati wa ile ahadi ambayo Mungu alimpa Ibrahimu ulipokuwa unakaribia, wale watu wakazidi na kuongezeka sana huko Misri,

18. hata mfalme mwingine akainuka juu ya Misri, asiyemfahamu Yusufu.

19. Huyo akawafanyia hila kabila yetu, na kuwatenda mabaya baba zetu, akiwaamuru wawatupe watoto wao wachanga, ili wasiishi.

20. Wakati huo akazaliwa Musa, naye alikuwa mzuri sana, akalelewa muda wa miezi mitatu katika nyumba ya babaye.

21. Hata alipotupwa, binti Farao akamtwaa, akamlea awe kama mwanawe.

22. Musa akafundishwa hekima yote ya Wamisri, akawa hodari wa maneno na matendo.

Mdo 7