Mdo 7:11-14 Swahili Union Version (SUV)

11. Basi kukawa njaa katika nchi yote ya Misri na Kanaani, na dhiki nyingi, wala baba zetu hawakupata chakula cha kuwatosha.

12. Hata Yakobo aliposikia ya kwamba huko Misri kuna nafaka, akawatuma baba zetu mara ya kwanza.

13. Hata safari ya pili Yusufu akajitambulisha kwa ndugu zake, jamaa ya Yusufu ikawa dhahiri kwa Farao.

14. Yusufu akatuma watu akamwita Yakobo babaye na jamaa zake wote pia, watu sabini na watano.

Mdo 7