18. Wakawaita, wakawaamuru wasiseme kabisa wala kufundisha kwa jina la Yesu.
19. Petro na Yohana wakawajibu wakawaambia, Kwamba ni haki mbele za Mungu kuwasikiliza ninyi kuliko Mungu, hukumuni ninyi wenyewe;
20. maana sisi hatuwezi kuacha kuyanena mambo tuliyoyaona na kuyasikia.
21. Nao walipokwisha kuwatisha tena wakawafungua, wasione njia ya kuwaadhibu, kwa sababu ya watu; kwa kuwa watu wote walikuwa wakimtukuza Mungu kwa hayo yaliyotendeka;
22. maana umri wake yule mtu aliyefanyiwa ishara hii ya kuponya ulipita miaka arobaini.