Mdo 4:18-22 Swahili Union Version (SUV)

18. Wakawaita, wakawaamuru wasiseme kabisa wala kufundisha kwa jina la Yesu.

19. Petro na Yohana wakawajibu wakawaambia, Kwamba ni haki mbele za Mungu kuwasikiliza ninyi kuliko Mungu, hukumuni ninyi wenyewe;

20. maana sisi hatuwezi kuacha kuyanena mambo tuliyoyaona na kuyasikia.

21. Nao walipokwisha kuwatisha tena wakawafungua, wasione njia ya kuwaadhibu, kwa sababu ya watu; kwa kuwa watu wote walikuwa wakimtukuza Mungu kwa hayo yaliyotendeka;

22. maana umri wake yule mtu aliyefanyiwa ishara hii ya kuponya ulipita miaka arobaini.

Mdo 4