19. Kwa hiyo, Ee Mfalme Agripa, sikuyaasi yale maono ya mbinguni,
20. bali kwanza niliwahubiri wale wa Dameski na Yerusalemu, na katika nchi yote ya Uyahudi, na watu wa Mataifa, kwamba watubu na kumwelekea Mungu, wakiyatenda matendo yanayopatana na kutubu kwao.
21. Kwa sababu ya hayo Wayahudi wakanikamata ndani ya hekalu wakajaribu kuniua.