Mdo 20:14-18 Swahili Union Version (SUV)

14. Alipotufikia huko Aso, tukampakia, kisha tukafika Mitilene.

15. Tukatweka kutoka huko, na siku ya pili tukafika mahali panapokabili Kio; siku ya tatu tukawasili Samo, tukakaa Trogilio, siku ya nne tukafika Mileto.

16. Kwa sababu Paulo amekusudia kupita Efeso merikebuni, asije akakawia katika Asia; kwa maana alikuwa na haraka, akitaka kuwahi Yerusalemu siku ya Pentekoste, kama ikiwezekana.

17. Toka Mileto Paulo akatuma watu kwenda Efeso, akawaita wazee wa kanisa.

18. Walipofika kwake, akawaambia,Ninyi wenyewe mnajua tangu siku ya kwanza nilipokanyaga hapa Asia, jinsi nilivyokuwa kwenu wakati wote,

Mdo 20