13. Wengine walidhihaki, wakisema, wamelewa kwa mvinyo mpya.
14. Lakini Petro akasimama pamoja na wale kumi na mmoja, akapaza sauti yake, akawaambia, Enyi watu wa Uyahudi, na ninyi nyote mkaao Yerusalemu, lijueni jambo hili, mkasikilize maneno yangu.
15. Sivyo mnavyodhani; watu hawa hawakulewa, kwa maana ni saa tatu ya mchana;