9. Bwana akamwambia Paulo kwa maono usiku, Usiogope, bali nena, wala usinyamaze,
10. kwa kuwa mimi ni pamoja nawe, wala hapana mtu atakayekushambulia ili kukudhuru; kwa maana mimi nina watu wengi katika mji huu.
11. Akakaa huko muda wa mwaka mmoja na miezi sita akifundisha kati yao neno la Mungu.
12. Hata Galio alipokuwa liwali wa Akaya, Wayahudi wakamwinukia Paulo kwa nia moja, wakamleta mbele ya kiti cha hukumu,
13. wakisema Mtu huyu huwavuta watu ili wamwabudu Mungu kinyume cha sheria.