13. wakisema Mtu huyu huwavuta watu ili wamwabudu Mungu kinyume cha sheria.
14. Na Paulo alipotaka kufunua kinywa chake, Galio akawaambia Wayahudi, Kama lingekuwa jambo la dhuluma au la hila mbaya, enyi Wayahudi, ingekuwa haki mimi kuchukuliana nanyi;
15. bali ikiwa ni hoja juu ya maneno na majina na sheria yenu, liangalieni ninyi wenyewe, maana mimi sitaki kuwa mwamuzi wa mambo hayo.
16. Akawafukuza waondoke mbele ya kiti cha hukumu.