49. Neno la Bwana likaenea katika nchi ile yote.
50. Lakini Wayahudi wakawafitinisha wanawake watauwa wenye cheo na wakuu wa mji, wakawataharakisha watu wawaudhi Paulo na Barnaba; wakawatoa katika mipaka yao.
51. Nao wakawakung’utia mavumbi ya miguu yao, wakaenda Ikonio.
52. Na wanafunzi walijaa furaha na Roho Mtakatifu.