Mdo 13:49-52 Swahili Union Version (SUV)

49. Neno la Bwana likaenea katika nchi ile yote.

50. Lakini Wayahudi wakawafitinisha wanawake watauwa wenye cheo na wakuu wa mji, wakawataharakisha watu wawaudhi Paulo na Barnaba; wakawatoa katika mipaka yao.

51. Nao wakawakung’utia mavumbi ya miguu yao, wakaenda Ikonio.

52. Na wanafunzi walijaa furaha na Roho Mtakatifu.

Mdo 13