Mdo 11:25-30 Swahili Union Version (SUV)

25. Kisha akatoka akaenda Tarso kumtafuta Sauli;

26. hata alipokwisha kumwona akamleta Antiokia. Ikawa kwa muda wa mwaka mzima wakakusanyika pamoja na kanisa na kuwafundisha watu wengi. Na wanafunzi waliitwa Wakristo kwanza hapo Antiokia.

27. Siku zizo hizo manabii walitelemka kutoka Yerusalemu hata Antiokia.

28. Na tulipokusanyika akasimama mmoja wao, jina lake Agabo, akaonyesha kwa uweza wa Roho Mtakatifu kwamba njaa kubwa itakuja karibu katika dunia nzima, nayo ikatukia katika siku za Klaudio.

29. Na wale wanafunzi, kila mtu kwa kadiri ya alivyofanikiwa, wakaazimu kupeleka msaada kwa ndugu zao waliokaa Uyahudi.

30. Wakafanya hivyo, wakawapelekea wazee kwa mikono ya Barnaba na Sauli.

Mdo 11